Mon, 8 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu Simba imethibitisha usajili wa kiungo Debora Fernandez Mavambo aliyekuwa akitandaza soka Ligi Kuu ya Zambia.
Ni kiungo mwingine anayetua kuzidi kuimarisha eneo hilo ambalo sasa limesheheni mafundi.
Ni mzaliwa wa Congo Brazaville lakini pia ana uraia wa Ghabon ambapo ameitumikia timu ya Taifa ya nchi hiyo.
Debora ni kiraka anayemudu kucheza nafasi yoyote katika eneo la kiungo. Ni moja ya sajili zilizokuwa zikisubiriwa kwa hamu kubwa na Wanamsimbazi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live