Thu, 15 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Simba wamefanikiwa kuondoka na alama tatu mbele ya JKT Tanzania baada ya kuwafunga 1-0.
Mbungi hiyo ya Ligi ya NBC imepigwa kwenye uwanja wa Meja Jenerali Semunho, Mbweni jijini Dar ambapo bao pekee la Simba lilifungwa na Clatous Chama dakika ya 33 ya mchezo.
Simba imefikisha alama 36 baada ya kucheza michezo 15 na sasa amebakiza alama 4 pekee kumfikia mpinzani wake Yanga ambaye anaongoza Ligi akiwa na alama 40.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live