Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba yaja na Sapraizi

Simba Baraza Data Simba yaja na Sapraizi

Wed, 17 Feb 2021 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

SIMBA inakuja na sapraizi nyingine kimataifa. Kitendo chao cha kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika pamoja na ushindi murua ugenini dhidi ya AS Vita Club umeongeza uwezekano mkubwa wa kuwa na timu nne msimu ujao.

Kufanya vizuri kwa Simba katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao, kwa kiasi kikubwa kutaiwezesha Tanzania kuwakilishwa na klabu nne katika mashindano ya klabu Afrika ambayo ni Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho Afrika.

Kwa mujibu wa mfumo wa ukokotoaji alama wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (Caf), hadi sasa kabla ya kuanza kwa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Tanzania ina nafasi ya kuingiza timu nne kutokana na kuwepo katika kundi la nchi 12 ambazo kila mmoja ina fursa ya kuwakilishwa na timu nne.

Tanzania ipo nafasi ya 12 ikiwa na pointi 15 ikichukua nafasi ya Libya ambayo iko nafasi ya 13 kwa idadi ya pointi 11 ilizonazo.

Pointi hizo zinaweza kuongezeka zaidi ikiwa Simba itamaliza angalau ikiwa nafasi ya tatu kwenye kundi au kufuzu robo fainali na hatua nyingine zaidi lakini kama itashika mkia kwenye kundi, mambo yanaweza kwenda tofauti kutokana na ushindani wa baadhi ya nchi ambazo zinanyemelea kuingia katika kundi hilo la nchi 12.

Libya timu yake ya Al Ahly Benghazi inaweza kuipiku Tanzania iwapo Simba haitofanya vyema kwenye makundi na yenyewe ikafika hatua za juu zaidi katika Kombe la Shirikisho Afrika.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz