Sat, 12 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bao pekee la Pape Ousmane Sakho dakika ya 63 linawapa Simba alama 3 mbele ya Ihefu mchezo wa Ligi Kuu ya NBC leo Novemba 12.
Mchezo huo uliopigwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa uliwashuhudia Simba wakikumbana na upinzani mkali kutoka kwa vijana wa Juma Mwambusi huku muda mwingi wakiutumia kujilinda.
Kwa ushindi huo Simba inasogea mpaka nafasi ya pili nyuma ya vinara Azam FC, katika msimamo wa Ligi wakijikusanyia alama 21 baada ya michezo 10.
Aidha Kocha wa Simba Juma Mwambusi bado ameendelea kulalamikia ufinyu wa ratiba kwa mechi zinazohusu kikosi chake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live