Mon, 22 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Simba Sc imeibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya klabu ya El Qanah katika dimba la Old Suez Canal kwenye mchezo wa kirafiki uliopigwa huko Misri.
FT: EL QANAH 0-3 SIMBA SC
14’—⚽️ Jean Ahoua
16’—⚽️ Jean Ahoua
120’—⚽️ Augustine Okejepha.
Mchezo huo uliochezwa kwa vipindi vitatu vya dakika 40' kufanya jumla ya dakika 120 ni mwanzo wa maandalizi ya Wekundu hao wa Msimbazi kuelekea msimu mpya wa 2024/25.
El Qanah ni Klabu inayoshiriki Ligi daraja la pili nchini Misri na kwenye ligi yao wamemaliza wakiwa nafasi ya 10 kwenye michezo 28 waliyocheza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live