Thu, 14 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Msaidizi wa Simba SC, Seleman Matola amesema wamefanyia kazi eneo lao la ulinzi hivyo kesho hawatarajii kuruhusu goli watakapopepetana na Mashujaa FC.
Matola ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumzia maandalizi ya mchezo huo utakaopigwa kesho Marchi 15, 2024 kwenye Uwanja wa Azam Complex- Chamazi jijini Dar majira ya saa 2:15 usiku.
"Ni kweli katika michezo yetu mitatu iliyopita karibu kila mchezo tumeruhusu goli, tumeliona hilo na tumelifanyia kazi hilo hivyo nia dhabiti kwa kesho ni kutoruhusu goli," alisema Matola.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live