Wed, 31 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ofisa habari wa Simba SC Ahmed Ally amethibitisha majeraha ya mlinda mlando wao namba moja Ayoub Lakred aliyoyapata Misri walipokita kambi ya maandalizi ya msimu mpya wa mashindano 2024-2025
"Ni kweli Ayoub ameumia paja na atafanyiwa vipimo atakaporejea kujua kama atatibiwa kawaida ama kwa njia ya upasuaji , madaktari bado hawajasema atakaa nje kwa muda gani, lakini itafahamika mara tu vipimo vitakapokamilika" Ahmedy Ally
Kikosicha Simba kinarejea nchini hii leo kikitokea Misri ilipoweka kambi ya wiki 3.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live