Thu, 22 Aug 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Yanga SC, Eng. Hersi Said amesema kuwa wanachama wa Klabu ya Simba walifanya uamuzi sahihi wa kumchagua Murtaza Mangungu kuwa mwenyekiti wao.
Kupitia kipindi cha Jana na Leo cha Wasafi Media, Eng. Hersi Said amesema; “Wanachama wa Simba wamemchagua Mangungu kuwa Mwenyekiti wa klabu na mimi naheshimu hayo maamuzi.
"Mimi niwaombe Simba wasije wakamuacha Murtaza Mangungu, ni kiongozi mzuri sana na ninaamini atawafikisha Simba kwenye nchi ya ahadi, kama ambavyo amefanya kwenye hii misimu mitatu iliyopita amefanya vizuri sana,” amesema Eng. Hersi Said.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live