Mon, 11 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Simba SC wametua nchini wakitokea nchini Morocco walipokuwa wamekwenda kukipiga na Wydad AC na kupokea kichapo cha 1-0.
Simba watajiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya NBC utakaopigwa Ijumaa hii Desemba 15, 2023 katika uwanja wa Uhuru jijini Dar dhidi ya Kagera Sugar.
Akimalizana na Kagera, Simba atarejea tena Klabu Bingwa kuindaa kucheza tena na Wydad mchezo nne wa Makundi katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar.
Kwenye kundi B, Simba wanashika mkia wakiwa na alama 2 huku vinara wakiwa na ASEC Mimosas wenye alama 7 wakifuatiwa na Jwaneng wenye alama 4 na Wydad akiwa na alama 3.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live