Fri, 2 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi, Simba SC, wamerejea kwenye Uwanja wa MO Simba Arena kwa ajili ya kuanza mazoezi kabla ya kuvaana na Polisi Tanzania pamoja na Coastal Unioni.
Simba wamerejea mazoezini jana Juni 1, 2023 chini ya Kocha Mbrazili Roberto Oliviera 'Robertinho'.
Taarifa waliyoiposti kwenye Simba App, Simba watacheza na Polisi Tanzania Juni 6 huku ile ya Coastal wakicheza Juni 9 na mechi zote wakiwa nyumbani ikiwa ni michezo ya kukamilisha Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2022-23.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live