Sat, 11 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha Simba leo kimefanyiwa vipimo vya Covid-19 ili kutambua hali zao za kiafya kuhusu ugonjwa huo ikiwa ni sehemu ya kuchukua tahadhari.
Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) limeweka utaratibu wa kabla ya mchezo wowote lazima kufanyike vipimo vya Covid-19 ili kuchukua tahadhari ya ugonjwa huo ambao ulitikisa dunia.
Hata hivyo, hakuna cha kuhofia kwa kuwa hakuna yeyote miongoni mwao kwenye msafara wao ambaye ameonyesha dalili za ugonjwa huo lakini kwa kuwa ni takwa la kikanuni kutoka CAF hivyo lazima tufanye.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live