Mon, 8 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi Simba SC, wamemtambulisha rasmi winga wao mpya Ladack Chasambi akititokea Mtibwa Sugar.
Vigogo wa Simba walikamilisha usajili wa winga huyo mapema Desemba mwaka jana na ilikuwa inebaki kumtangaza.
Chasambi amepandishwa Mtibwa Sugar msimu huu kutoka timu ya vijana ya U20 inayoshikilia ubingwa wa Ligi ya umri huo kwa msimu wa tano mfululizo.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Mtibwa, zimefichua kuwa, Simba imekubali kununua mkataba wa miaka miwili aliokuwa nao Chasambi na klabu ya Mtibwa, kisha fasta ikamalizana na Mchezaji Bora huyo wa U20 2023.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live