Mon, 27 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Afisa Habari wa Yanga SC, Ally Kamwe amesema juzi taifa liliingia aibu baada ya Simba kupata sare na ASEC Mimosas na mashabiki kuingia wachache uwanjani.
Kamwe alisema, kwa kulitambua hilo, mashabiki wa Yanga watawaonesha ni namna gani uwanja unatakiwa ujae Jumamosi hii watakapokuwa wanacheza na Al Ahly katika Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar.
"CAF wasifikiri labda kuna msiba kwa kuona wameingia mashabiki 66 kwenye ule mchezo, sisi tutaujaza uwanja kurejesha heshima maana sisi ndio wenye mpira huu nchini," alisema Kamwe.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live