Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba walifanikiwa hapa kwa Azam FC

Ngoma Fredy .jpeg Simba walifanikiwa hapa kwa Azam FC

Fri, 10 May 2024 Chanzo: George Ambangile

Aina ya mechi ambayo ilikuwa inahitaji nani atatumia nafasi zake? Maana ilikuwa wazi sana, spaces zipo nyingi sana, ni ishu ya nani atakuwa mfanisi zaidi ya mwenzak, na Simba SC alikuwa mfanisi zaidi ya Azam FC

Simba SC ni kama walijua wachezaji wote wa mbele wa Azam FC ukiacha Feisal ni wanapenda mpira mguuni (ball to feet) badala ya kuwa runners na ndio maana walikuwa wanakabia katikati zaidi (Midblock) wanawaacha Fuentes na Bangala wawe na mali lakini ikifika tu katikati ya uwanja wanafika.

Shida ya Azam dhidi ya Midblock ya Simba ni kukosa runners, kwanini kwasababu

1: Bin Yazd, Bangala, Fuentes na Akaminko walikuwa wanapewa muda na nafasi kwenye mpira kilichotakiwa?

2: Ni wachezaji wa mbele wa Azam kufanya runs nyuma ya safu ya ulinzi ya Simba space nzuri ilikuwepo.

Ukibadilisha meza, ndio kitu ambacho Simba SC waliwafanyia Azam, kwasababu Chilambo na Msindo walikuwa wanahama sana kusogea juu maana yake kuna spaces nzuri pembeni ya uwanja.

1: Fred baki ndani dhidi ya Bangala na Fuentes

2: Chasambi na Balua fanya runs nje ya mabeki wawili wa kati wa Azam kwasababu fullbacks hawapo wapo juu

3: Simba walifanya hivi mechi nzima kipindi cha kwanza na cha pili ilikuwa ishu ya kutoa adhabu stahiki tu.

4: Kipindi cha pili Simba waliongeza juhudi kubwa sana ya kushinda mipira ya pili mingi pamoja na kushinda mipambano yao .

NOTE

1: Energy ya Mzamiru na Kanoute katikati leo ilimpa msingi mkubwa Ngoma apige pasi zake

2: Kipre dribbling zake zinakuvutia kucheza rafu, ngoma alikuwa muhanga

3: Kwenye mechi kama hizi ukipata nafasi usipotumia, utakuja kuadhibiwa wewe waulize Azam.

4: Hawa vijana wavumilieni, tuendelee kuwapa muda: Msindo, Chilambo, Chasambi, Balua, Israh.. watafika tu, ishara ipo

5: Zimbwe Jr MR RELIABLE

FT: Azam FC 0-3 Simba SC

Chanzo: George Ambangile