Wed, 21 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Meneja wa timu ya Simba SC, Mikael Igendia amesema nahodha wa timu John Bocco hakuwa sehemu ya msafara kwa sababu ya majeraha.
Igendia amefunguka hayo akiwa nchini Ivory Coast ambako timu imewasiri kuwakabili ASEC Mimos kesho kutwa Ijumaa Februari 23.
"Wachezaji watatu muhimu ambao hatujasafiri nao ni Ayoub Lakred, Willy Onana na John Bocco ambaye alipata majeraha tulipokuwa tunashiriki Kombe la Mapinduzi," alisema Igendia.
Meneja huyo alisema Bocco atakapopona majeraha yake, atajiunga na timu na wenzake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live