Wawakilishi wa Tanzania katika Michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika, Timu ya Simba SC imefanikiwa kuondoka na alama tatu muhimu dhidi ya Vipers ya Uganda.
Mchezo huo wa Hatua ya Makundi umepigwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Bao pekee la ushindi katika mchezo huo limefungwa na kiungo Clatous Chotta Chama dakika ya 45+1.
Kwa ushindi huo Simba wanakwea mpaka nafasi ya pili katika msimamo wa kundi C, hivi sasa wakiwa na alama 6 nyuma ya Raja Casablanca.
Mpaka sasa msimamo upo hivi;
KUNDI C
1. Raja Casablanca — 12pts
2. Simba SC — 6pts
3. Horoya AC — 4pts
4. Vipers SC — 1pts