Fri, 5 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi, Simba inashuka dimbani leo kuikabili APR ya Rwanda katika mchezo wa kukamilisha hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Mapinduzi.
Mchezo huo wa kundi B kwenye uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar utafuatia mchezo wa awali kati ya Jamhuri na Jamus.
Simba inaongoza kundi hilo ikiwa na poiti sita baada ya michezo miwili ikifuatiwa na Singida Fountain Gate yenye pointi sita michezo mitatu, APR ikishika nafasi ya tatu ikiwa na pointi tatu baada ya michezo miwili wakati JKU ni mwisho haina pointi baada ya michezo mitatu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live