Wakati waamuzi wa mechi ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika baina ya Simba na Orlando Pirates, Jumapili Aprili 17 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa wakiwekwa hadharani, Simba imeruhusiwa kuingiza jumla ya mashabiki 60,000 katika mchezo huo.
Idadi hiyo ndio ukomo wa mwisho wa namba ya mashabiki ambao Uwanja wa Benjamin Mkapa inaweza kuingiza katika mechi moja.
Habari za uhakika kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) na lile la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) zimefichua kuwa Simba imeruhusiwa kuingiza idadi hiyo ya mashabiki baada ya kupeleka ombi CAF.
"Simba wameruhusiwa kuingiza jumla ya mashabiki 60,000 Jumapili, Aprili 17 katika mechi yao dhidi ya Orlando Pirates," kilithibitisha chanzo chetu.