Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba ni Chama, Bocco tu

Simba Chama Pic 2 Data Simba ni Chama, Bocco tu

Wed, 16 Dec 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

Kasi ambayo Yanga inaenda nayo kwenye Ligi Kuu Bara msimu huu ni kama inawavuruga mabingwa watetezi wa ligi hiyo Simba, ambao juzi walipata ushindi kiduchu wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City.

Licha ya Mbeya City kuwa ya tatu kutoka chini ya misamo wa ligi, iliibana Simba katika mchezo huo na kama ingeongeza kasi kidogo mchezo ungemalizika kwa sare.

Simba inacheza mechi zake katika presha ya kutetea ubingwa wao na kusaka taji la nne mfululizo la ubingwa msimu huu, huku kasi ya wapinzani wao wakubwa, Yanga ambayo imeanza kufunga idadi kubwa ya mabao katika mechi zake ikizidi kuwachanganya.

Miamba hiyo imezidiwa na Yanga pointi nane, huku pia ikiwa na mechi mbili mkononi za viporo dhidi ya KMC wanayocheza nayo Jumatano na dhidi ya Dodoma Jiji ugenini.

Ukiondoa mechi hizo, Simba ina mechi nne, mbili za kumaliza mzunguko wa kwanza wa ligi dhidi ya Namungo iliyopangwa kufanyika Jumapili na dhidi ya Azam itakayofanyika Desemba 27, wakati watani zao, Yanga wakiwa na michezo miwili dhidi ya Dodoma Jiji (Desemba 19) na itamaliza mzunguko wa kwanza kwa kucheza na Ihefu ugenini Desemba 26.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz