Wed, 5 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Klabu ya Simba Juma Mgunda amesema kuwa wanaelekeza nguvu zao zote kwenye mchezo wa ligi ya Mabingwa dhidi ya Premiero De Agosto ya Angola.
Mgunda amesema kuwa maandalizi dhidi ya De Agosto yameanza mara moja na mapungufu yaliojitokeza kwenye mchezo na Dodoma Jiji yatafanyiwa kazi mazoezini kabla ya kukutana wapinzani wao mwishoni mwa juma lijalo.
“Maandalizi ya mchezo huo tayari yameanza na kitu kizuri hatutakuwa na mchezo wa ligi hivyo tutapata muda wa kufanya marekebisho yaliyojitokeza mazoezini,”amesema Mgunda.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live