Wed, 5 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Vigogo wa Kariakoo, Simba SC na Young Africans SC ndiyo watafungua pazia a Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao wa 2024/25 katika mchezo wa nusu fainali ya Ngao ya Jamii.
Kwa mujibu wa kanuni za Ligi Kuu Tanzania bara, michezo ya Ngao ya Jamii itazikutanisha timu (4), ambapo Bingwa wa Ligi Kuu msimu wa nyuma (yaani msimu huu) atacheza na mshindi wa tatu (3), wakati mshindi wa pili (2) atakutana na mshindi wa nne (4).
◉ Young Africans vs Simba SC. ◉ Azam FC vs Coastal Union.
Bado Shirikisho la Soka Tanzania kupitia Bodi ya Ligi halijataja uwanja gani utakaotumika katika michezo hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live