Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba na Yanga kukutana kundi moja CAFCL?

Yanga X Simba Balaa Simba na Yanga kukutana kundi moja CAFCL?

Mon, 2 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Tanzania imeweka historia kwa mara ya kwanza timu zake mbili kutinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, hii ni baada ya mapacha wa Kariakoo, Simba SC na yanga Sc kufanikiwa kutinga hatua hiyo kwa pamoja ndani ya msimu mmoja.

Yanga wametinga hatua hiyo maada ya kushinda hatua ya kwanza ya awali kwa kuifunga ASAS FC ya Djibouti kwa mabao 2-0 ugenini na 5-1 nyumbani (jumla ya bao 7-1), kisha hatua ya pili ya awali kuwafunga Al-Merrikh ya Sudan mabao 2-0 ugenini na bao 1-0 nyumbani (jumla ya bao 3-0).

Kwa upande wa Simba SC wao hawakuanzia hatua ya mwanzo, badala yake walianzia hatua ya pili ya mtoano na kutoa sare ya bao 2-2 ugenini dhidi ya Power Dynamos na jana wakatoa sare ya bao 1-1 wakiwa nyumbani (jumla ya sare 3-3) hivyo wamefanikiwa kuingia makundi kwa kanuni ya bao la ugenini.

Msimu uliopita, Simba ilikuwa hatua ya Makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo ilitolewa katika hatua ya robo fainali baada kwa mikwaju ya peanti dhidi ya Raja Casablanca.

Yanga wao msimu uliopita walicheza mpaka fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika na kuibuka washindi wa pili kwa kanuni ya bao la ugenini baada ya kutoa sare ya bao 2-2 na USM ALger ya Algeria.

Simba na Yanga wanaweza kukutana kwenye hatua ya Makundi ya michuano hiyo kwani Simba wapo Pot namba 2 wakati Yanga wakiwa pot namba ipo Pot 3, hivyo kuna uwezekano mkubwa wa miamba hao wa soka nchini Tanzania kukutana kwenye kundi moja.

Draw ya CAF CL & CC Itafanyika Ijumaa, October 6 Johannesburg Africa Kusini, Kila timu imepangwa kwenye POT yake kutokana na wingi wa alama zake kwa kipindi Cha miaka mitano [5] iliyopita.

Simba POT 2 [35]

Yanga POT 3 [20]

Timu 15 mpaka sasa zimeshafuzu hatua ya Makundi ya CAFCl na bado timu moja tu inayosubiriwa baada ya mchezo wa leo kati ya CR Belouizdad na Bo Rangers ambapo matokeo ya mchezo wa awali Bo Rangers ilifungwa bao 3-1.

Al Ahly

Pyramids

Jwaneng Galaxy

TP Mazembe

Petro Luanda

ES Tunis

Medeama

Mamelodi

Yanga SC

Etoile Sahel

Wydad AC

Simba SC

ASEC Mimosas

Al Hilal

Nouadhibou

Belouizdad or Bo Rangers

Yanga yenyewe itakuwa chungu cha tatu na timu za TP Mazembe, Al Hilal na Asec Mimosas.

Kwa mujibu wa kanuni za mashindano hayo, kila kundi litaundwa na timu moja kutoka kila chungu kati ya vinne ambavyo vitakuwepo katika uchezeshaji wa droo na hakuna zuio kwa timu za nchi mmoja kukutana.

"Chama cha mpira hakiwezi kuwa na timu zaidi ya mbili kutoka nchini mwake kwenye hatua ya makundi," inafafanua kanuni ya 3 ibara ya 17 ya mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

CAFCL Group Stage

#POT1

Al Ahly - Misri

Wydad AC - Morocco

Esperance Tunis - Tunia

Mamelodi Sundowns - Afrika Kusini

#POT2

CR Belouizdad - Algeria

Pyramids FC - Misri

Petro Atletico - Angola

Simba SC - Tanzania

#POT3

TP Mazembe - Congo DR

Al Hilal SC - Sudan

Yanga SC - Tanzania

ASEC Mimosas - Ivory Coast

#POT4

Etoile Sahel - Tunisia

Jwaneng Galaxy - Botswana

FC Nouadhibou - Mauritania

Medeama SC - Ghana

Kundi atakalokuwepo Simba na atakalokuwepo Yanga litakua na mpinzani mmoja kutoka hapa.

1. Al Ahly SC

2. Wydad Casablanca

3. Esperance de Tunis

4. Mamelodi Sundowns

Haitokuwa jambo la kushangaza ikiwa Yanga na Simba zitakutana katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwani imeshawahi kutokea mara nyingi nyuma kwa timu za nchi moja kukutana katika hatua hiyo.

Tangu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika ianzishwe rasmi mwaka 1998, misimu 10 tofauti imeshuhudiwa timu za nchi moja kukutana katika hatua ya makundi.

Sudan na Misri ndio zinashikilia rekodi ya nchi ambazo klabu zake zimekutana mara nyingi zaidi katika hatua ya makundi ambapo kwa Sudan timu za Al Hilal na Al Merrikh zimekutana mara tatu ikiwa ni msimu wa 2021/2022, 2017 na 2009, kama ilivyo kwa Misri katika msimu wa 2012, 2010 na 2008.

Mara mbili tofauti, timu za Tunisia zilikutana katika hatua ya makundi kama ilivyo kwa Algeria wakati DR Congo na Angola timu zake zimewahi kukutana mara moja kwa kila nchi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live