Ofisa Habari wa Klabu ya Yanga, Ally Kamwe amewasihi mashabiki wa Simba kutoenda uwanjani na mawazo ya kuwapiga/kuwashambulia viongozi wao iwapo watafungwa kwenye mchezo wao wa dabi, Jumamosi Aprili 20.
Kamwe amesema hayo baada ya baadhi ya mashabiki kudai kuwa iwapo watafungwa na watani zao Yanga katika mchezo huo, basi watawashushia kipigo viongozi wao wa Simba humo humo kwenye Dimba la Benjamin Mkapa.
Simba kwa sasa wanapitia wakati mgumu baada ya kucheza mechi nne mfululizo bila kushinda huku wakitolewa kwenye michuano ya CAFCl na Kombe la Shirikisho Tanzania.
"Ni tabia ya kishamba mpira umeisha mnawapiga viongozi, achaneni nayo njooni tuangalie mpira. Tuliwapiga tano mkaondoka vizuri tu majumbani kwenu njooni mungalie mpira.
"Tukishinda sisi tutawatania mkitufunga tutaondoka nyumbani, lakini msije na 'mentality' kwamba Yanga wakitufunga humu ndani kunakuwa uwanja wa vita hapana," amesema Ally Kamwe.