Kikosi cha Simba SC, kinatarajia kuondoka jijini Dar kesho Jumanne Marchi 5, 2024 kwenda kuwasubiri Tanzania Prisons wakipige Jumatano Marchi 6, 2024.
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema wachezaji wanatarajia kuondoka kesho majira ya saa 4 asubuhi jijini Dar na wakifika watapumzika na Jumatano watakuwa dimbani kumkabili Tanzania Prisons.
"Tunafahamu Prisons wameimraika sana siku za hivi karibuni, tunafahamu wamekuwa wakifunga sana lakini sisi tumejiandaa kuhakikisha hatuchafui furaha yetu tuliyonayo baada ya ushindi wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Jwaneng Galaxy," alisema Ahmed.