Klabu ya Simba SC imepeleka ofa ya Geita Gold, ikimtaka mshambuliaji Valentino Mashaka katika usajili wao wa kuelekea msimu ujao.
Timu hiyo imepanga kufanya maboresho katika kikosi chake kwa kuiboresha safu hiyo ya ushambuliaji inayochezwa na Omar Pa Jobe na Fred Koublan.
Simba ikipanga kusajili wachezaji hao wapya pia imepanga kuachana nao baada ya msimu huu kutokana na kushindwa kuonyesha.
Kwa mujibu wa mmoja wa mabosi wa Simba, ameliambia Championi Ijumaa kuwa wapo katika mazungumzo ya mwisho katika kuipata saini ya mshambuliaji huyo, ambaye ameonyesha kiwango bora msimu huu.
Kwa undani zaidi fuatilia Gazeti la Championi kupitia Global App au Rifary.