Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba kumalizia hasira zote kwa Ihefu

Makamanda Simba SC 1140x640 Simba kumalizia hasira zote kwa Ihefu

Fri, 11 Nov 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Baada ya sare ya bao 1-1 waliyoipata kwenye mchezo wao uliopita dhidi ya Singida Big Stars, Kocha wa Simba, Juma Mgunda ameweka wazi kuwa mechi yao ijayo dhidi ya Ihefu FC itakuwa ni ya kurekebisha makosa ya mechi iliyopita.

Kesho Jumamosi Simba watashuka dimbani kucheza na Ihefu kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.

Mgunda alisema kuna kila sababu ya wao kupata ushindi kwenye mechi yao ijayo kwa kuwa tayari wamepoteza alama mbili kwenye mechi iliyopita na wanatakiwa kufanya kila kinachowezekana ili kushinda dhidi ya Ihefu.

Mgunda alisema: “Tumefanya makosa kwenye mechi iliyopita na tunakubali kwa sababu imeshatokea na hakuna namna ya kuweza kuubadilisha ukweli. Lakini tunatakiwa kurekebisha hayo kwenye mchezo ujao.

“Tukubali kuwa kuna makosa yalifanyika kwenye upande wetu na sisi kama benchi la ufundi tunakwenda kukaa chini na kuyarekebisha haraka kabla ya kwenda uwanjani.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live