Wekundu wa Msimbazi Simba SC, wanatarajia kushuka dimbani Desemba 26, 2023 kula kiporo chake dhidi ya Mashujaa FC.
Mchezo huo wa raundi ya 6, Simba atakuwa mgeni wa Mashujaa katika uwanja wa Lake Tanganyika.
Simba akicheza mchezo huo atakuwa amelingana na Yanga kwa kucheza michezo 10 michezo lakini siku hiyo hiyo, Yanga ataanza kucheza mchezo wa raundi ya 11 dhidi ya Kagera Sugar.
Kwenye msimamo mpaka sasa kabla ya mechi hizo, Yanga ana alama 27 akiwa nafasi ya pili huku Simba akiwa na alama 22 akiwa nafasi ya tatu. Nafasi ya kwanza inashikiliwa na Azam FC ambao wana alama 28 wakiwa mbele kwa michezo, wamecheza michezo 12.