Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba kujiuliza mbele ya Azam FC

Azam Vs Simba HT Simba wataikaribisha Azam FC katika dimba la Mkapa

Mon, 20 Feb 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Simba SC inatarajia kucheza mchezo wake wa ligi dhidi ya Azam FC baada ya kutoka kupoteza michezo miwili mfululizo ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.

Simba wapo nafasi ya pili kwenye msimamo wa NBC baada ya kucheza michezo yake 22, wakiwa wameshinda michezo 16, sare 5 na kupoteza mchezo 1 hadi sasa wakiwa wamejikusanyia pointi zao 53.

Wakati kwa upande wa Azam FC wao wanashikilia nafasi ya nne, wakiwa wameyoka kupoteza michezo miwili mfululizo kwenye ligi, huku wakiwa wameshinda 13, sare 4 na kupoteza mara 5.

Mechi ya kwanza walipokutana, Mnyama alipoteza kwa bao 1-0 ambalo walifungwa na Prince Dube lililoifanya timu hiyo kuondoka na pointi tatu. Je Mnyama kesho atakubali kupoteza tena mbele ya Azam?

Chanzo: www.tanzaniaweb.live