Mchambuzi wa soka, Amri Kiemba amesema, mashabiki wanapaswa kuelewa kwamba Simba SC imebaki kwenye ubora iliokuwa nao lakini Yanga imepanda kuwafikia.
Mchambuzi huyo ametoa kauli hiyo jana kwenye uchambuzi wake redioni.
“Simba wamebaki palepale lakini watu wanataka Simba itoke pale iende mbele zaidi, Yanga imepanda na kuifikia Simba, hii inafanya Yanga ionekane imefanya kazi kubwa sana.”
“Yanga imepanda juu na kufikia daraja la Simba ukilinganisha na lile gap la awali hiyo ndio inafanya watu waone Simba haifanyi kitu, wanaiangalia Yanga.”
“Watu wanaona Simba imeshuka kuja ilipo Yanga lakini kumbe Yanga ndio imepanda na kuifikia Simba.”