By OLIPA ASSAWACHEZAJI wa Tanzania Prisons, Lambert Sabiyanka (straika) na Salum Kimenya (kiungo), wamefichua siri ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba, kwamba imetokana na kujua ubora na mapungufu ya wapinzani wao.
Wameliambia Mwanaspoti jana Alhamisi ya oktoba 22, mwaka 2020 mara baada tu ya kumaliza mechi hiyo, iliyopigwa Uwanja wa Nelson Mandela, uliopo mkoani Rukwa, kwamba baada ya kujua mambo hayo mawili, walicheza kwa nidhamu kubwa.
Sabiyanka amesema licha ya kuwafunga, Simba sio timu ya kuibeza, amefafanua ina wachezaji makini na kwamba hilo walilijua mapema ndio maana waliamua kuwaheshimu na kujua ni namna gani wanaweza wakapata matokeo mazuri.