Mchambuzi wa masuala ya soka nchini kutoka East Africa Radio, Samwel Rashid mwenyewe anajiita Wakanda Republic amesema kuwa wachezaji wa Kikosi cha Simba hakuna hata mmoja ambaye anaweza kuingia kwenye kikosi cha kwanza cha Yanga.
Wakanda amesema hayo wakati akizungumzia mchezo wa Simba dhidi ya Yanga ambapo Wananchi waliibuka na ushindi mnono wa bao 5-1, Novemba 5, 2023 katika Dimba la Mkapa.
"Ukisema uchukue Marking scheme, uifanye Yanga iwe Marking Scheme ya kikosi cha Simba, yaani tutaanza kuchambua hapa tutafika hatua tutaona hamna mchezaji wa Simba hata mmoja ambaye anafaa kukaa hata kwenye benchi Yanga, yaani hiyo ni by Fact," amesema Wakanda.