Mdau wa soka na mdhamini wa jezi ya Simba, Sandaland amesema: "Mechi ya Simba na Yanga ni dabi kubwa na ni waasisi wa ligi ya Tanzania, hivyo klabu zetu zinaweza zikanuifaka kwa kuuza jezi.
"Nitumie nafasi hii kuwatangazia mashibiki wa Simba kwamba wajitokeze kwa wingi wakiwa wamevaa jezi za Simba na gari la kuziuza jezi hizo litakuwepo Benjamin Mkapa na wanaponunua ni kwa manufaa ya klabu, hilo pia niishauri Yanga kwamba wanaweza wakatumia mchezo kuuza jezi zao."
Sunderland amebainisha hayo, Novemba Mosi 2023 wakati akichangia mada kwenye mjadala wa Mwananchi Space, mada isemayo Simba, Yanga zitumiaje dabi ya Kariakoo kibiashara.