Mon, 11 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi Simba SC na watani wao wa jadi Yanga SC, wikiendi hii wanarejea kwenye ligi kuu ya NBC kutupa karata zao baada ya kutoka kwenye mechi zao za kimataifa.
Ijumaa Desemba 15, 2023, Simba watakuwa nyumbani kuwakaribisha Kagera Sugar katika Uwanja wa Uhuru huku Yanga wakiwakaribisha Mtibwa Sugar Jumamosi Desemba 16, 2023.
Kwenye msimamo, Simba wapo nafasi ya tatu wakiwa na alama 19 wakiwa wamecheza mechi 8 huku nafasi ya pili ikishikiliwa na Yanga ambao wana alama 24 wakiwa wamecheza mechi 9.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live