Sat, 11 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mechi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara baina ya watani wa jadi, Simba na Yanga imemalizika kwa sare ya bila mabao jioni hii Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Kwa sare hiyo, Yanga SC inafikisha pointi 20 na kuendelea kuongoza ligi kwa pointi mbili zaidi ya mabingwa watetezi, Simba SC baada ya wote kucheza mechi nane.
Mchezo huo baina ya watani ulitwaliwa zaidi na ufundi wa hali ya juu kutoka kila upande.
Walinda milango wa pande zote mbili walifanya kazi kubwa kwa kuokoa michomo kadhaa iliyoelekezwa katika himaya zao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live