Wed, 22 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Simba imeuhamisha Mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya klabu ya KMC kutoka uwanja wa Azam Complex hadi Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha Tanzania. Mchezo wa kwanza ambao KMC walikuwa nyumbani katika uwanja wa Azam Complex ulimalizika kwa sare (2-2) dhidi ya Simba SC.
Taarifa kutoka Simba App imesema;
"Arusha tunakuja Mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya KMC utapigwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha siku ya Jumamosi Mei 25, 2024 saa 10:00 jioni. Taarifa zaidi kwenye Simba App. #WenyeNchi #NguvuMoja."
Chanzo: www.tanzaniaweb.live