Mon, 6 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Wanawake ya Simba, Simba Queens safari yake imekwama hii leo baada ya kupokea kipigo cha 2-1 Vihiga Queens katika mchezo wa nusu fainali.
Kipigo hicho walichokipata Simba Queens kinahitimisha safari yao katika Mashindano ya CAF Women’s Champions League CECAFA Qualifiers kwa mwaka huu 2021.
Mchezo huo ulipigwa katika dimba la Nyayo stadium na kuwaacha Simba Queens wakishuhudia Vihiga Queens wakitinga hatua ya fainali ya michuano hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live