MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Bara, Simba wanatarajia kushuka visiwani hapa Januari 4 kwa ajili ya kuanza kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi ambalo litaanza kurindima Januari 2 mwakani.
Timu hiyo iliyopangwa kundi C la kombe hilo itafika siku hiyo huku Januari 5 watashuka uwanjani kuvaana na Selem View mechi itakayopigwa saa 10:15 jioni.
Nusu fainali ya mashindano hayo makongwe visiwani hapa itapigwa Januari 10 huku fainali yake ikitarajiwa kupigwa Januari 13.
MAKUNDI MAPINDUZI CUP
KUNDI A
Azam
Namungo
Yosso Boys
Meli 4 City
KUNDI B
Yanga
Taifa Jang’ombe
KMKM
KUNDI C
Selem View
Simba
Mlandege