Meneja wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally akizindua tawi la Simba Kigamboni jioni hii, ameulizwa yanayoendea kuhusu mchezaji wao, Clatous Chota Chama ambaye amesajiliwa na Yanga.
"Mashabiki wa Simba wapo wanaosema tutangaze mapema Thank you ya Chama, wengine wanasema tutangaze mapema kama anabaki Simba SC.
"Ndugu zangu Chama yupo mioyoni mwetu na tunakiri tunapenda sana, hatutaki tufanye maamuzi ambayo yatatuumiza baadae ndio mana mnaoa tuko kimya katika sku hizi, bado viongozi wanaongea nae.
"Mnapaswa kujua, ikiwa Chama atabaki ni kwa maslahi ya Simba na kama akiondoka ni kwa maslahi ya Simba.
"Chama sio kama wachezaji wengine. Angekuwa mchezaji wa kawaida kawaida kama wengine mpaka ninavyozungumza nanyi sasa hivii tungekuwa tayari tumemgonga Thank You. Kwa hiyo tuwe wavumilivu," amesema Ahmed Ally.