Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba, KMC ngoma ngumu

Simba Kmc Pic Data Simba, KMC ngoma ngumu

Wed, 16 Dec 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

Dar es Salaam. Baada ya moto wao kushindwa kudhibitiwa katika mechi tatu zilizopita za Ligi Kuu, John Bocco na Clatous Chama leo wana fursa nyingine ya kuthibitisha ubora wao wakati Simba itakapoivaa KMC kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia saa 1.00 usiku.

Wawili hao katika michezo mitatu iliyopita ya Simba dhidi ya Coastal Union, Polisi Tanzania na Mbeya City, wamehusika katika mabao nane kati ya 10 ambayo Simba imefunga.

Bocco, ambaye anaongoza katika ufungaji akiwa na mabao nane, amefunga mabao manne katika mechi tatu zilizopita, akipachika matatu dhidi ya Coastal Union na lingine dhidi ya Mbeya City wakati Chama akifunga manne, amefunga mabao mawili katika kila mechi dhidi ya Polisi Tanzania na Coastal Union.

KMC haina rekodi nzuri mbele ya Simba, wamepoteza mechi zote nne walizowahi kukutana katika Ligi Kuu, wakifunga mabao mawili, wakiruhusu nyavu zao kutikiswa mara nane.

Timu hizo zinakutana zikiwa katika kiwango na ubora wa hali ya juu, zimekuwa na matokeo ambayo hayapishani sana katika michezo mitano iliyopita.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz