Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba: Haikuwa bahati, tumemwaga jasho la kutosha

Simba Kuvuja Jasho Simba: Haikuwa bahati, tumemwaga jasho la kutosha

Sat, 6 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Simba imeeleza kuwa haikuwa bahati kwao kufuzu nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika licha ya wachezaji wa timu hiyo kumwaga jasho jingi kwa ajili ya nembo ya timu yao .

Simba imeondoshwa na Al Ahly kwa jumla ya mabao 3-0 baada ya jana usiku kukubali kichapo cha mbao 2-0 huko nchini Misri katika mchezo wa robo fainali mkondo wa pili.

Kupitia ukurasa wa Instagram wa timu hiyo wamechapisha ujumbe wenye kutia moyo wachezaji pamoja na mashabiki wa Simba huku wakipania michuano mingine iliyosalia.

"Mashujaa wetu walipambania nembo ya Simba na Tanzania lakini bahati haikuwa kwetu. Kimataifa tumemaliza lakini mashindano ya ndani yanaendelea, nguvu zetu tunahamishia huko ili kufanya vizuri."

Chanzo: www.tanzaniaweb.live