Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Shirika la ndege la Morocco kufanya Safari 30 kuwabeba mashabiki Qatar

Shirika La Ndege La Morocco Kufanya Safari 30 Kuwabeba Mashabiki Qatar Shirika la ndege la Morocco kufanya Safari 30 kuwabeba mashabiki Qatar

Tue, 13 Dec 2022 Chanzo: Bbc

Shirika la ndege la Morocco, Royal Air Maroc litafanya safari za ndege 30 maalum kuwabeba mashabiki wa soka kutoka Casablanca hadi Doha kwa mchezo wa Jumatano wa nchi hiyo wa nusu fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya Ufaransa, shirika hilo la ndege lilisema Jumatatu.

Ndege hizo zitaondoka Jumanne na Jumatano, ilisema.

Kwa furaha ya Wamorocco, na sio tu mashabiki wa soka, nchi hiyo imekuwa ya kwanza barani Afrika kufuzu kwa nusu fainali ya Kombe la Dunia.

Abiria katika safari za bei ya chini ya kwenda na kurudi wataongeza kwa maelfu ya raia wa Morocco ambao tayari wanahudhuria mashindano ya soka huko Doha.

Chanzo: Bbc