Mon, 25 Jan 2021
Chanzo: habarileo.co.tz
Katibu wa Shirikisho la Vyama vya Tiba Asili nchini, Othaman Shem ameomba Serikali kuangalia upya uwezekano wa kupunguza gharama kubwa ya usajili wa dawa za asili.
Shem ametoa wito huo mkoani Morogoro kwenye maonesho ya mimea dawa kwa wadau wa tiba za asili yaliyoandaliwa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).
“Gharama kubwa za usajili wa dawa za asili imekuwa ni kikwazo kwa wataalamu wa tiba asili kuweza kuingiza dawa hizo kwenye soko la ndani nan je ya nchi," amesema Shem.
Chanzo: habarileo.co.tz