Mon, 26 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Winga wa klabu ya Al Ahly, Hussein El Shahat raia wa Misri ameongeza mkataba mpya wa miaka mitatu kuendelea kuitumikia klabu hiyo mkataba ambao utaisha mwaka 2026.
El Shahat mwenye umri wa miaka 31 alikuwa analipwa mshahara wa dola 83,000 (zaidi ya Milioni 190 za Kitanzania) kwa mwezi
Baada ya kuongeza mkataba mpya kwa sasa atakuwa analipwa mshahara wa dola 100,000 (zaidi ya milioni 230 za Kitanzania) kwa mwezi na kuwa miongoni mwa wachezaji wanaolipwa mshahara mkubwa Al Ahly sawa na Percy Tau raia wa Afrika Kusini na Ali Maaloul raia wa Tunisia wanaolipwa mshahara huo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live