Kamati ya Madili ya TFF, imemmfungia mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho Hilo, Mwanahabari Shaffih Dauda kujihusisha na masuala ya Soka ndani na nje ya nchi kwa miaka mitano na kulipa faini ya shilingi milioni 6.
Shaffih amekumbana na adhabu hiyo baada ya kuchapisha taarifa ya uongo kuhusu TFF kupitia Akaunti yake ya Instagram Februari 8 mwaka huu.
Aidha , Kamati hiyo imemfungia maisha kujihusisha na mpira wa Miguu Mjumbe wa kamati ya Utendaji ya Biashara United Hawaiju Gantala baada ya kupeleka masuala ya soka katika mahakama za kawaida akipinga Uchaguzi wa Biashara United Mara kuendelea.
Tazama hapa chini Taarifa za kufungiwa kwao;