Haya ni maelezo yangu nikifafanua ninachokiamini kwa haya maamuzi yaliyofanywa na Simba siku ya jana,masaa chini ya 48 tangu Simba waliposhushiwa kichapo cha mabao 5-1 kutoka kwa mtani wao Yanga SC .
Ukweli ni kwamba kipigo hiki kimeeavuruga viongozi kwa sehemu kubwa , presha ya mashabiki kwenda kwa viongozi pia ni kubwa hivyo viongozi wametafuta wakumpa hili zigo ili kuhamisha focus .
Robertinho aliiongoza Simba kwenye mechi za mashindano mengine [Azam Sports Federation Cup na Ngao ya Jamii]. Na hizi ni namba zake
AZAM SPORTS FEDERATION CUP
Mei 6, 2023 Azam FC 2-1 Simba
NGAO YA JAMII
Agosti 10, 2023 Simba 0-0 Singida Fountain Gate [P 4-2]
Agosti 13, 2023 Yanga 0-0 Simba [P 1-3]
Alipoteza mechi moja ya ASFC, akashinda kwa mechi mbili za Ngao ya Jamii kwa changamoto ya mikwaju ya penati na kufanikiwa kuchukua Ngao ya Jamii.