Thu, 9 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wakati Mashabiki wa Simba wakitishia kuanza maandamano ili kushinikiza uongozi kujiuzulu baada ya Simba kupokea kichapo cha mabao 5-1 kutoka kwa Yanga.
Mchambuzi wa Michezo kutoka Clouds FM Shaffih Dauda amesema huu sio wakati wa Simba kufanya vurugu na badala yake waungane na kuisapoti Tmu katika kipindi hiki.
Akizungumza Shaffih anasema;
“Mambo ya kuandamana hayana mpango wowote , kama kuandamana wangeandamana Manchester United huko kwa hiki wanachopitia ,kazi ya shabiki ni kuisapoti timu yake , Manchester United wanafungwa na mechi ijayo wanaenda uwanjani kwa wingi ule ule “
Chanzo: www.tanzaniaweb.live