Tue, 15 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya kuonesha kiwango bora kwenye ‘mechi’ yake ya kwanza ya 'Ligi' dhidi ya Al-Raed, Mwandishi wa Habari na shabiki wa klabu ya Al-Ittihad, Ibrahim Al-Faryan hakufanya hiyana kumpa zawadi ya saa aina ya Rolex mchezaji wa zamani Liverpool, Fabio Henrigue Tavares, Fabinho
Kiungo huyo alicheza ‘mechi’ yake ya kwanza ya ‘Ligi’ ya Saudi Pro, usiku wa kuamkia leo, na kuisaidia ‘timu’ yake hiyo kupata ushindi wa mabao 3-0.
Fabinho alijiunga na Al Ittihad kwa mkataba wa pauni milioni 40, na kuungana na nyota wengine kama Karim Benzema, Ngolo Kante.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live