Nyota wa #RealMadrid, Vinicius Junior ametoa pongezi kwa Klabu ya #Sevilla kwa kuchukua hatua za haraka za kumtoa uwanjani na kumripoti kwa Mamlaka Shabiki wake kwa madai ya kumtusi na kumbagua kwa rangi Vinicius
Taarifa ya Sevilla baada ya mchezo baina yake na Real Madrid, uliomalizika kwa sare ya 1-1, imeeleza;
"Kuna mtu alitambuliwa akifanya vitendo vya ubaguzi, alitolewa nje ya uwanja na kukabidhiwa kwa Mamlaka ya Kisheria. Baada ya hapo atachukuliwa hatua zikiwemo za kufukuzwa Uanachama kwa kuwa Klabu inalaani tabia yoyote ya ubaguzi wa rangi na chuki.”
Ndani ya kipindi cha Miezi 12 iliyopita, #ViniciusJr amekuwa mwathirika wa Matukio 7 ya Ubaguzi wa Rangi kutoka mashabiki wa Timu mbalimbali za #Spain hasa #AtleticoMadrid.