Wed, 9 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais Mstaafu wa FIFA, Sepp Blatter amesema ilikuwa ni makosa kuipa Qatar uenyeji wa Kombe la Dunia kwa sababu nchi hiyo ni ndogo kuliko ukubwa wa mashidano hayo.
Uamuzi huo ulifanyika mwaka 2010 wakati Blatter akiwa madarakani, lakini amesema yeye aliipigia kura Marekani huku aliekuwa Rais wa UEFA akiipigia Qatar.
Michuano ya Kombe la Dunia 2022 inaanza Novemba 20 nchini Qatar na itamalizika Disemba.
Qatar imetajwa kuvunja haki za binadamu wakati wa utengenezaji wa viwanja vinavyotajwa kutumika kwa mechi za Michuano ya Kombe la Dunia, hali kadhalika hali mbaya ya hewa nchini humo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live