Fri, 25 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ushindi wa mabao 3-1 walioupata Simba wa Teranga, Timu ya Senagal dhidi ya wenyeji Qatar umeibua matumaini kwa Kikosi hicho kufuzu kwa hatua ya 16 bora Michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Qatar.
Kichapo hiko kinatoa picha mbaya kwa wenyeji wa mashindano hayo Timu ya Qatar kuondolewa hatua ya makundi baada ya kupoteza mchezo wa pili kati ya mitatu hatua ya makundi.
Magoli ya Senegal yamefungwa na B. Dia 41', F. Diedhiou 48 ' na B. Dieng dakika ya 84 ya mchezo wakati bao pekee la Qatar katika michuano hii likifungwa na Muntari dakika ya 78.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live